TANNAH Why Me cover image

Paroles de Why Me

Paroles de Why Me Par TANNAH


Alhamdullilahi maana siku imekucha
Namshukuru Mungu siku nyingine kunipa
Naongea peke yangu ka kichwani na kikao
Why? Nalalia mkeka wenzangu wanalalia mbao

Umri unakwenda na nishakuwa mtu mzima
Boyfriend naye aliyenichokoza 
Naye ana gari la kwazima
Kaliona dimbwi kumbe urefu wa kisima

Nashangaa walikula mbegu
Na wakataka wakate shina
Safari ni ndefu na dereva hajui njia
Japo nimekosa seat ila mimi bado ni abiria

Sina kitu ya nini niruke kiwanja
Mtoto wa kanjanja na home sure kapanda
Sijawai hata kutishwa kuhofia mikwara
Walosema akili ni nywele walinishauri ninyoe kipara
Moyo kidonda bado natibu makovu
Yaani sina umuhimu kama sabuni liloishiwa povu

Mi ngali mwana mkiwa la kaa moja 
Sometimes -- patupu
My mama told me niongeze imani 
Kwa kumuomba Mungu ehaa
Nilishikwa ndoa ila sasa ndoano
Shimoni huku nitoe baba nishike mkono
(Nishike mkono)

Umasikini ni ugonjwa usio na chanjo
Na ndugu wamejawa lawama na masimango
Kwa kumwamini yupi? Ikiwa rafiki wa karibu
Anaweza kuwa mpango wa kando wa mume wako bila aibu

Nachoamini mi nitapata japo muda sio sasa
Maisha zaidi ya jela yanafunza yananyanyasa
Yasikie ila usiombe yakakukuta
Unaeza juta kukuta goigoi kaangusha ukuta

Nafsi inasema Tannah kaza huna simple
Na hapo ulipo ndipo matatizo napo yapo
Kila nikiwaza mi ni mwanamke
Ila ni baba nafosi kujaza na kijai kibaba

Mbona itakuwa mchicha kuwa mbuyu
Leo Temeke, Tanga kesho, kutwa Tukuyu
Nikifumba macho usidhani nimelala
Kuishi na watu kazi tena isiyo na mshahara

Mi ngali mwana mkiwa la kaa moja 
Sometimes -- patupu
My mama told me niongeze imani 
Kwa kumuomba Mungu ehaa
Nilishikwa ndoa ila sasa ndoano
Shimoni huku nitoe baba nishike mkono
(Nishike mkono)

Dunia imenielemea
Binadamu hawa wanananionea
Rupia nayo imenigomea
Sasa niende wapi mama?

Why me? Maswali mengi najiuliza
Why me? Tatizo nini?
Umasikini utaniua mimi

Mi ngali mwana mkiwa la kaa moja 
Sometimes -- patupu
My mama told me niongeze imani 
Kwa kumuomba Mungu ehaa
Nilishikwa ndoa ila sasa ndoano
Shimoni huku nitoe baba nishike mkono
(Nishike mkono)

Nitoe Baba, nitoe nitoe

Ecouter

A Propos de "Why Me"

Album : Why Me (Album)
Année de Sortie : 2020
Copyright : (c) 2020
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : May 05 , 2020

Plus de Lyrics de TANNAH

TANNAH
TANNAH
TANNAH

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl