STORI ZA KAPEDO Wajinga Nyinyi  (Part 6) cover image

Paroles de Wajinga Nyinyi (Part 6)

Paroles de Wajinga Nyinyi (Part 6) Par STORI ZA KAPEDO


Hello mum, I hope uko poa
Mi niko tu bado nang'ang'ana
Si ni wewe unilinifunza nizoee kukula jasho langu
Ju crime si poa
Na mi bado najikaza kisabuni lakini bado siwezi afford soap
Sijui kama umeona kwa news vile watu wanabebwa na maji
Unajua mbona? Ni ju pesa ingetengeneza drainage system
Iliflow kwa mifuko za watu, I mean, ilikunywa maji
Na imekuwa ngumu kupata justice ju ukihire lawyer wananunua judge
Saa hii ukiuliza kesi ya Sharon iliendaje?
Utaskia Ooo-Bado tunafuatilia

By the way mum, after kumaliza shule nilipata kazi
Na ni ya kutafuta kazi 
Si unajua ukiwa na kazi siku hizi hiyo si kazi
Kazi ya kutafuta kazi ndio kazi lakini ukiwa na connections sio kazi kupata kazi
Enyewe if education is the key then heri wote tungesomea kuwa key cutter ama fundi wa locks
Ju graduation parties zimejazana maua lakini huku nnje maisha sio bed of roses

Wale wanasema vijanaa tujiajiri wameajiriwa
Mum tuliamka mapema tukapigia hawa politicians kura ndio wapite
Siku hizi kwa traffic ni siren wakituharass ndio wapite
Wapite? Ndio wafike kwa parliament walale 
I guess ndio maana wako na pay sleep 

Depression imefanya wazazi ndio wanazika watoto
Na cost of living iko high mtu hata hawezi afford kamba ya kujinyonga
Naskia mtoto hajazaliwa ako na deni China 
Na kesho headlines zitasema uchumi imepanda
Imepanda? Ni sawa tu Mungu anawaona

Cheki, si ati na dis-respect the dead 
Lakini mheshimiwa akikufa na Cancer ni headline
Mwananchi akikufa na Cancer inakuwa statistics tu
Btw mahindi ina aflotoxin iliingiaje kwa port?
Kama sio mtu alipewa za macho ndio afunge macho
Siku hizi hadi siasa inapigwa kwa mazishi
Na wakipatana ni kurushiana maneno na matusi haziishi
Ona wanasubiri sportsmen wakufe ndio wakawacelebrate kama heroes
Ni sawa tu Mungu anawaona

Mum, is it true that mtu akiwa na pesa anaweza nunua justice?
Mbona tunasahau siri ni kama mimba ata uifiche aje itajitokeza
If politicians ndo wasemaji wetu, niambie tuligeuka bubu lini
Si niheri tujifunze sign language tupige kelele nayo
Niambie kama vijana ndio leaders wa tomorrow, kesho ni lini?
Ni ukweli kuna pesa ilipotelea Afya House ndio maana mwananchi hana good health care?
Na mheshimiwa akipata homa anakuwa airlifted  na ndege
Huku treatment anapelekwa abroad

Ni ukweli zile wheelbarrow walinunua 100k zilikuwa za kutubeba wana  
Ni swali tu, ati bado kuna IDps kwa camp wakati politicians wanagrab mashamba
Ati kuna politician alibebwa na ndege akafungue class imejengwa na matope
Aii mum sio sawa, hawa politicians wanalalia King Size bed
Wakati hospitals zina admit watu wawili kwa kitanda moja
Ni sawa tu Mungu anawaona

(Mum kata simu kwanza wacha niongee na hawa mapoliticians one on one)

Nyinyi mapolitician wakati wa kupiga kuta tulimark tik
Kumbe tunamake wrong choices
Cheki mmegeuka viziwi hata parliament iwe na speaker hamskii
Mlienda sherehe bunge that's why mlitaka tuwachague via political parties
Angalia hatuko mbele pamoja ni kama tulifananisha ndimu na chungwa
Ju speed ya maendeleo kwa ground sio chap chap
Na shuku ni ju tulichoose governor
Siku ya mwizi ni arubaini lakini ya politician ni siku bond imekatika
Human rights ni upande wa kulia, rip Willy Kimani
Whistle blower wamekatiwa pumzi 
Msidhani nitachicken out bila kumention ile stori ya chicken

Cheki tunaishi maisha ya hand to mouth ni kama body parts zingine hazina maana
Hivi hii ndo motherland yenu, mbona watoto wenu wanaenda majuu for further studies
Angalia mmetuwachia school motto na baridi ya ujinga inafreeze brain ya watoto
Hata tuchange syllabus, mnatusoma mnaprove sisi ndio silly basi
Wapi hiyo spirit ya Mau Mau if tuko busy tunauma uma mali ya umma
Cheki tunageuka banana republic mahali kuna political party ya chungwa
Kama ni pudding mlitaka si mngesema mapema 
Anthem inasema tuwe na plenty within our borders 
Wakati mmejaa dream ya kushika passports mkaishi majuu

Na kwa boy wa ghetto, greener pastures ni akina veve tu
Na visa anatambua ni kisa za rape na wizi wa kimabavu
Na kanisa siku hizi zinaongozwa na dad and mums
But hawako willing kufungulia milango street children
Ni sawa tu Mungu anawaona

Ecouter

A Propos de "Wajinga Nyinyi (Part 6)"

Album : Wajinga Nyinyi (Part 6) (Single)
Année de Sortie : 2020
Copyright : (c) 2020
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : Jan 20 , 2020

Plus de Lyrics de STORI ZA KAPEDO

STORI ZA KAPEDO

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl