GOODLUCK GOZBERT Nyakati cover image

Paroles de Nyakati

Paroles de Nyakati Par GOODLUCK GOZBERT


Unaona kama kila unachoguza kimeharibika
Ujasiri wa kusema tena umetoweka
Maana kila unalosema wewe kama unakosea
Umechanganyikiwa ni Mungu ajua unayopitia

Na ukisema ueleze, wengi kwao ni furaha
Wewe mwombe Mungu ubaki kimya
Na mengi umevumilia, moyo umenyong'onyea
Hapo ulipo sasa ng'ang'ania tena


Na Mungu hajaruhusu, jaribu kuliko uwezo wako
Imani nusu ongeza utashinda
Mungu hatoruhusu ufe kabla ya baraka zako
Imani nusu ongeza utashinda

Mmmh, 
Zipo nyakati za furaha
Nawe utacheka tena, usijali, Mungu yupo nawe
Zipo nyakati za furaha
Nawe utacheka tena, usijali, Mungu yupo nawe

Mmmh, 
Moyo wako una majeraha haufai
Tena unasubiri kauli ya mwisho ya Mungu
Wapo wanaojua we huna mtoto
Kwa kejeli wanaulizaga ana umri gani?
Tena wanaojua umefukuzwa kazi
Kwa kejeli wanaulizaga Bosi wako yupo?

Ila nakwambia hayatodumu ni nyakati tu
Hautobaki hapo haya ni mapito, 
Jipe moyo tazama juu mwombe Mungu ujasiri
Ni mapito tu jipe moyo mkuu
Japo huna nguvu ya kumwomba 
Mwishie Mungu, ni mapito tu
Jipe moyo mkuu

Mungu hajaruhusu, jaribu kuliko uwezo wako
Imani nusu ongeza utashinda
Mungu hatoruhusu ufe kabla ya baraka zako
Imani nusu ongeza utashinda
Nawe utacheka tena usijali Mungu yupo nawe

Mmmh, 
Zipo nyakati za furaha
Nawe utacheka tena, usijali, Mungu yupo nawe
Zipo nyakati za furaha
Nawe utacheka tena, usijali, Mungu yupo nawe

Wewe...
Oooh oooh...
yeah yeah heeh

Hata wakizusha maneno ya uongo 
Wakakwambia umemuasi Mungu
Ni sawa hawajui unakopita
Wakaja na unabii wakasema umefika mwisho wako wewe
Ni sawa hawajui unakopita

Wakainuka ndugu wa karibu wakakusema ovyo ovyo
Ni sawa hawajui unakopita
Ikawa kila kitu ni kimya, marafiki ni kimya
Ni sawa hawajui unakopita
Kama ndoa ni yako lakini ndani ni uadui
Ni sawa hawajui unakopita

Zipo nyakati za furaha
Nawe utacheka tena, usijali, Mungu yupo nawe
Zipo nyakati za furaha
Nawe utacheka tena, usijali, Mungu yupo nawe

Zipo nyakati za furaha
Nawe utacheka tena, usijali, Mungu yupo nawe
Zipo nyakati za furaha
Nawe utacheka tena, usijali, Mungu yupo nawe

Ecouter

A Propos de "Nyakati"

Album : Nyakati (Single)
Année de Sortie : 2019
Copyright : (c) 2019
Ajouté par : Huntyr Kelx
Published : Mar 18 , 2019

Plus de Lyrics de GOODLUCK GOZBERT

GOODLUCK GOZBERT
GOODLUCK GOZBERT
GOODLUCK GOZBERT
GOODLUCK GOZBERT

Commentaires ( 0 )

Aucun commentaire pour l'instant



A propos de AfrikaLyrics

Afrika Lyrics est la plus large collection de paroles de chansons et de traductions d’Afrique. Afrika Lyrics fournit les paroles des musiques de plus de 30 pays africains et des traductions de lyrics de plus de 10 langues africaines en français et en anglais.

Suivre Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl