Kifo Lyrics by TOXIC


Nilishajua nikifa nitaona sana masnitch
Baba yangu ni swala tano ila nje kumbe nje ana binti
Rafiki yangu na dem wangu wajaa laana wote wanancheati
Mkeka nilobetigi kabla sijafa naona umetiki

Natamani ningerudi ila mwili hautamaniki
Au kama vipi naomba hata nikatoe laumu mama na ziki 
Niliacha mdogo wa kike nikahisi mama atamkomboa
Kumbe niliacha una mimba leo umekwenda kuitoa

Kinachoniuma sio poa alompa mimba 
Muuza sumu ya panya na dawa ya madoa
Kumbe ndoa it means alifanya kwa akili yake 
Unajiuliza ama ali-, ama ni ziki 
Ama ni tamaa kampitia ibilisi

Vituko vyangu na utani na ucheshi
Vinafanya mtaani kwetu watu wengi wakikumbuka wanimiss
Ata Ex wangu kaipost ile picha yangu mbaya kuliko zote
Ati kuniwish mi ni rest in peace

Ni kama hukumu imekamilika
Shetani na jeshi lake, Mungu naamini
Majibu yake maumivu, mmmh
Yawezekana leo nikawa superstar na attention
Kesho nikala madawa, chizi kwa meditation
Hello, my Lord Hello ooh!

Na siku ya kufa imewekwa fumbo ambalo huwezi ukafumbua
Ndo maana ukifumba macho huwezi tena ukafumbua
Utapambwa kwa mazuri japo baya wanajua 
Na wema wako unazidi ubaya wako unapungua

Simu yangu inapigwa sana siwezi ipokea
Na ni wale wasiojua kitu kilonitokea
Yule jamaa anayenidai ananifokea 
'Missed call na message zote why you don't care?

Na akijua atakwenda kwenye msiba 
Nako hakuna hata wa kumlipa 
Hali ngumu atawachanganyia stress nyingine 
Kuniwaza mimi deni lake sijui atae jivika hili jukumu

Labda angejivika mjomba ila nae anamsomesha binamu
Na yuko chuo hana mkopo wala boom
Oh daa! Sina tena cha kusema zaidi ya kuwaaga goodbye
Muda wangu umeniishia kuishi huku

Ni kama hukumu imekamilika
Shetani na jeshi lake, Mungu naamini
Majibu yake maumivu, mmmh
Yawezekana leo nikawa superstar na attention
Kesho nikala madawa, chizi kwa meditation
Hello, my Lord Hello ooh!

Watch Video

About Kifo

Album : Kifo (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jul 13 , 2021

More TOXIC Lyrics

TOXIC

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl