Raha Lyrics by NEEMA MWAIPOPO


Adui zangu, nimewasamehe bure
Na moyoni mwangu sina kinyongo tena
Watesi wangu nimewasamehe bure
Na moyoni mwangu, nimejaza msamaha

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Matukio ni mengi katika dunia
Na wanaotuudhi ni wengi mno
Na wengine ni wale wa karibu nasi
Tutaweka wangapi katika mioyo

Matukio ni mengi katika dunia
Na wanaotuudhi ni wengi mno
Na wengine ni wale wa karibu nasi
Tutaweka wangapi katika mioyo

Mwisho mioyo yetu ipasuke bure
Mwisho sura zetu, zizeeke mapema

Mwisho mioyo yetu ipasuke bure
Mwisho sura zetu, zizeeke mapema
Rahaaaa jipe mwenyewe...

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Ugomvi ni mbaya, huumiza moyo
Kinyongo ni hatari, hukosesha raha
Kwa nini ujitese kwa mambo yapitayo
Hao ni wanadamu, wanapita tu

Ugomvi ni mbaya, huumiza moyo
Kinyongo ni hatari, hukosesha raha
Kwa nini ujitese kwa mambo yapitayo
Hao ni wanadamu, wanapita tu

Hata wasipotubu, wewe wasamehe
Usijinyime raha jipe mwenyewe

Hata wasipotubu, wewe wasamehe
Usijinyime raha, jipe mwenyewe
Nasema raha jipe mwenyewe...

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Adui zako, wewe wasamehe bure
Na moyoni mwako usiwe na kinyongo
Watesi wako we wasamehe bure
Na moyoni mwako ujaze msamaha

Binadamu wengine ni wakorofi
Hata ukinyamaza, watasema tu
Ajira yao kubwa ni masengenyo
Usigombane nao, utakosa nguvu

Binadamu wengine ni wakorofi
Hata ukinyamaza, watasema tu
Ajira yao kubwa ni masengenyo
Usigombane nao, utakosa nguvu

Ukifanikiwa wanakasirika
Kama waliyachangia, mafanikio yako
Mungu akikuinua mioyo inawauma
Kama walijuwa agano lako na Mungu
Ukifanikiwa wanakasirika
Kama waliyachangia, mafanikio yako
Mungu akikuinua mioyo inawauma inawakera
Kama walijuwa agano lako na Mungu
Mie Raha Najipa Mwenyewe...

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Usikubali moyo upasuke bure
Usikubali sura izeeke mapema
Usikubali moyo upasuke bure
Kisha sura izeeke mapema
Wewe raha jipe mwenyewe

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Moyo wangu una amani
Moyo wangu hauna mashaka
Moyo wangu una furaha
Moyo wangu hauna kinyongo

Watch Video

About Raha

Album : Raha (Single)
Release Year : 2015
Copyright : (c) 2021
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jan 16 , 2021

More NEEMA MWAIPOPO Lyrics

NEEMA MWAIPOPO

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl