NACHA Mdahalo cover image

Mdahalo Lyrics

Mdahalo Lyrics by NACHA


Hebu ngojeni kwanza acheni kucheza bao
Tufanye huu mdahalo kuhusu mambo kibao
Hivi kwani ndo ujanja siasa za majukwaa
Kuvua na nguo na kupaka 
Au ndo dalili ya ukomavu wa siasa

Nchi huru hii unafanya bwana unachotaka
Enhe Juma unasemaje eti una nini hapa?
Hizo ni njaa na ni tamaa za paka
Yaani barabarani chanzo chake ni nini?

Uzembe wa madereva na vitu vingi kichwani
Kwani matrafiki hawapo? Rushwa ni kufuru
Ah mbona siwaelewi? haipo takukuru?
Mfumo wa vyama vingi aloleta Nyerere
Mnauona unafanya kazi? Mmmh mipaka kengele
Hivi tutafuzu kombe la dunia kisha tunywe mvinyo?
Wabongo msahau hata kocha awe Mourinho

Kwa hio na mimi nikitaka madaraka naweza pata?(Eeeh....eeeh)
Alafu mkinata na simu nitakata(Aaah weee)
Mnaona vipi tukiishi bila dini matabaka(Eeeh....eeeh)
Hivi ni ungwana nikioa alafu kipigo talaka?(Aah aah weee)

Serikali ni watu na watu ndio sisi
Kwa hio nautamani urafiki wa raia na polisi
Mimba za utotoni? Nini unahisi?
Tatizo na watoto wanaponzwa sana na chipsi

Kama ni kweli basi hali inatisha
Nyie mnauona muungano wa zenji na Tanganyika?
Eeeh mbona bado upo hauoni Yanga fika
Mo banker Fei Makame bado anatisha

Hivi nilikuwa na wazo utani sesha swedi
Madada poa waruhusiwe ila walipe kodi
Alafu pesa zikasaidie wamama wodi
Hahaha hizo akili za ki odi

Mmmh dah, aisee wewe kwa hiyo walimu na madoctor 
Nani mshahara waongezewe?
Mmmh bora walimu ila madoctor nao wenyewe
Nchi ishauzwa nipeni mimi nikalewe

Kwa hio na mimi nikitaka madaraka naweza pata?(Eeeh....eeeh)
Alafu mkinata na simu nitakata(Aaah weee)
Mnaona vipi tukiishi bila dini matabaka(Eeeh....eeeh)
Hivi ni ungwana nikioa alafu kipigo talaka?(Aah aah weee)

Ni sawa Simba na Yanga vilabu kongwe vya soccer
Nikiwa na mtu mmoja kama Moa anavyotaka
Itapandisha soccer mfumo itaporomosha
Hio ni vita kubwa kuna watu riziki watakosa
Kwa mfano sasa, shule za kata ni ongezeko ufaulu
Ama bado zero nekta

Fullu kivipi? Wanafunzi mia sita 
Alafu walimu watano wacheni kujifurahisha
Haya si walimtukana mzee juzi walilia ka watoto
Hee si walimtukana mamba kabla hawajavuka mto?

Tena na hili linanichanganya kuhusu sisi vijana
Maambukizi ya zinaa na mipira mingi sana
Tunazidi kuungua kwa sababu ya uzembe sana
Aah soksi za nini na tumezaliwa peku
Mchungaji kula kondoo hio ni sawa bila wasi
Fisi akikosa nyama huwanga wanakula nyasi

Kwa hio na mimi nikitaka madaraka naweza pata?(Eeeh....eeeh)
Alafu mkinata na simu nitakata(Aaah weee)
Mnaona vipi tukiishi bila dini matabaka(Eeeh....eeeh)
Hivi ni ungwana nikioa alafu kipigo talaka?(Aah aah weee)

Mnyasubi ndani ya Mbanyu beiby
Wamemchokoza bear

Watch Video

About Mdahalo

Album : Mdahalo (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Feb 20 , 2020

More NACHA Lyrics

NACHA
NACHA
NACHA
NACHA

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl