Haijakaa Sawa Lyrics by MBOSSO


(Mocco)

Sasa una nuna nini?
Au unadhani hata mimi napenda
Nishazichoka na mimi
Mboga za majani kila siku mrenda

Siko juu siko chini
Niko nusu sado
Sio wa kumi si sabini
Ngoma ngumu bado

Kama ibada naswali sana
Usiku wa manane tena nafunga na suna
Mambo bado, bado mwana wane
Naona yanazidi kuvuma

Nikirudi na hasira hasira (Nizoee)
Mambo magumu bado bila bila (Niombee)
Nikirudi na hasira hasira (Nizoee)
Mambo magumu bado bila bila (Niombee)

Haijakaa sawa! 
Nivumilie ipo siku tutapata
Haijakaa sawa! 
Shida na dhiki zitakwisha beiby

Haijakaa sawa! 
Kucha na kope make-up utapaka
Haijakaa sawa! 
Tutabadili mboga kuku kwa manyama

Chochea kuni kipenzi changu
Asubuhi tumbo likikuminginya
Pokea kidogo changu
Tunywe chai kwa mkate wa kumimina

Akili ikichoka, riziki nikikosa
Najua kwako nitajiliwaza
Kama makosa nivute chumbani
Kununa nuna unajilemaza

Ustahimilivu mnao wachache mno
Jua shida rafiki wa mbivu
Baada ya dhiki mavuno
Kila jema lina maumivu

Na kwenye waliomo tumo
Yarabi salama tupe tulivu
Penzi lisifike kikomo
Iyee iyee

Nikirudi na hasira hasira (Nizoee)
Mambo magumu bado bila bila (Niombee)
Nikirudi na hasira hasira (Nizoee)
Mambo magumu bado bila bila (Niombee)

Haijakaa sawa! 
Nivumilie ipo siku tutapata
Haijakaa sawa! 
Shida na dhiki zitakwisha beiby

Haijakaa sawa! 
Kucha na kopa make-up utapaka
Haijakaa sawa! 
Tutabadili mboga kuku kwa manyama

Watch Video

About Haijakaa Sawa

Album : Haijakaa Sawa (Album)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020 Wasafi Records.
Added By : Huntyr Kelx
Published : Mar 22 , 2020

More MBOSSO Lyrics

MBOSSO
MBOSSO
MBOSSO
MBOSSO

Comments ( 1 )

.
6137 2020-04-18 05:59:55

Mbosso is a genius Afrikan legend in the making I love this Afrikan brother of mine continue shining the true son of the land



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl