Kitoroli Lyrics by KAREN


Umeniburuza ka kitoroli
Kutwa kunipeleka puta
Ile sandaka lawe

Ukaniona mpori pori
Kukupenda ukavimba kichwa
Leo bora ninawe

Sikudhani siku moja
Kama nitakuja toa machozi
Kwa ajili yako na nilalame
Iyeee

Kukuganda ka ruba 
Kuonyesha upendo hukujali 
Kabisa maa ee, ooh maa eeh

Natembelea magongo (Aaah)
Mzima bado nachechema (Aah)
Ila kwa hali sio shwari

Nisije nikatoka chongo
Kwa mapenzi kung'ang'ana
Nikadhoofu hali

Nalia mwenyewe, mwenyewe
Japo nina ugonjwa moyoni sijui lini nitapona
Nalia mwenyewe, mwenyewe
Mgonjwa nakatisha dozi bora nitoweke duniani

Nalia mwenyewe, mwenyewe
Mgema kasifiwa pombe kaitia maji nanyotokwa
Nalia mwenyewe nitazoea hali yangu

Don't cry beiby, we unadhani itakuaje 
Ukiondoka ukasepa na moyo wangu mfa maji
Don't cry beiby, we unadhani itakuaje 
Ukiondoka ukasepa na moyo wangu mfa maji

Si unataka kunitosa
Na unajua mapenzi hayana kocha (Kweli nimekubali)
Najua umechoka
For the first time natambua makosa (Kweli nimekubali)

Mwisho wa wiki hazikuniisha safari
Vishawishi kasababisha dosari
Najikuta nagonganisha magari
Oooh mama ma

Hapo sasa umenishika sharubu
Tungi tungi nyumbani 
Unafanya kusudi kunisulubu
Tumpe faida nani?

Mdomo juu juu unataka niwe bubu
Siwezi kukuchapa makofi utakuwa sugu
Kwanza mapenzi matamu kati ni msala
Unapopungua upendo na kugeuka bishara
Kosa pesa ulale kwenye kochi
Kodoa macho tochi

Nalia mwenyewe, mwenyewe
Japo nina ugonjwa moyoni sijui lini nitapona
Nalia mwenyewe, mwenyewe
Mgonjwa nakatisha dozi bora nitoweke duniani

Nalia mwenyewe, mwenyewe
Mgema kasifiwa pombe kaitia maji nanyotokwa
Nalia mwenyewe nitazoea hali yangu

Watch Video

About Kitoroli

Album : Kitoroli (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : Jun 04 , 2020

More KAREN Lyrics

KAREN
KAREN
KAREN

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl