K2GA R.I.P JPM  cover image

R.I.P JPM Lyrics

R.I.P JPM Lyrics by K2GA


Tanzania mmmh

Ni wewe, shujaa wetu 
Ni wewe, mjasiri wetu
Ni wewe ulotupa nuru watanzania
Komanda wetu

Ni wewe, shujaa wetu 
Ni wewe, mjasiri wetu
Ni wewe ulotuonyesha njia watanzania
Komanda wetu

Umetutoa kwenye kiza
Ukatuvuta mikono ukatuleta kwenye taa
Na ukatukogesha sasa twapendeza tena tunang'aa
Miaka mitano ikapita, na mengine tukakupa we

Imani yetu furaha yetu ukiongoza Tanzania
Ulipokuja ulituambia hapa kazi tulisisitizia
Umeondoka umetuacha kimya kimya hata kutuambia
Bendera imetulia wananchi tunakulilia wee
Viongozi wamejiinamia hatuna la kufanya Mungu kashaamua

Ni wewe aah, ni wewe uuh
Ni wewe Magufuli tunakulilia
Baba ni wewe, ni wewe uuh
Ni wewe kweli umetuacha peke yetu Tanzania

Tulikuita chuma, shujaa 
Mkombozi wa wanyonge
Tena uliweka njia pasipokuwa na njia
Viongozi wa bongo majibu ukayatuma
Ukaweka nguvu ipate kukua 
Hakuna kama wewe nani asiyekujua

Hivi mnakumbuka juzi tu Dodoma aliapa
Kwamba atashika miaka mitano tulompatia
Ndo kwanza miezi sasa hata mwaka mmoja hujafika
Mama Samia ametangaza Rais Magufuli ametangulia

Ni wewe aah, ni wewe uuh
Ni wewe Magufuli tunakulilia
Baba ni wewe, ni wewe uuh
Ni wewe kweli umetuacha peke yetu Tanzania

 

Watch Video

About R.I.P JPM

Album : Angerudi (Single)
Release Year : 2021
Copyright : (c) 2021 Kings Music.
Added By : Huntyr Kelx
Published : Mar 18 , 2021

More K2GA Lyrics

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl