Kiwembe Lyrics by JOH MAKINI


Wananiita Mr Mstaarabu
Ninachongoja misa na ni sababu
Nishawekeza hisa ya hii dhahabu
Ndoa ndo imani msingi wa dhawabu

Uadilifu hauhofii uajibikaji
Usiri ndo sera mama ya uekezaji
Usivujishe usivujishe
Maskani mingi hatarishi

I wish, natamani ushindani usitoke nnje
I wish, tukikujaga zamani hakuna ubishi
Jiko lipikalo maajabu enjoy mapishi
Tamaa udhaifu, mtaji ni uaminifu

Na nguzo hii huwa sipenyi mchwa wala siafu
Mechi za kirafiki nimestaafu
Hapa ndio kikomo cha usaili
Sihitaji mtu wa kati hii ni kati yetu sisi wawili

Leo nafanya usajili wa ligi ya maisha
Walisha niita kulipwa kimataifa
Nishapiga nyingi ridhaa sikuwa na manufaa
Leo timu yetu ni familia makini mama

Vile inafaa umezaliwa super mi niongezwe star
Uitwe 'superstar' ju ya vile ninakaa vizuri
Tuweke history, wataka this story 
Mwambie mweusi ni pori, shore 

Walishazushaga kuniita kiwe-kiwembe
Sasa wametuliza mawe-mawenge
Umbea kwa vituo bama, vya mwenge
Habari zipo kwetu mnara wa wenge

Walishazushaga kuniita kicheche
Sasa wametuliza mawenge
Umbea kwa kituo bamaa vya mwenge
Yelele lile

Sio kila kitu kwangu ila ni kitu changu kizuri
Mechi ni kali naikaba mpaka kivuli
Sitaki fanya bahati wala siiti ngekewa
Ulipo nilipo ndipo tulipotakiwa kuwa

Mama utakula vingi Musa alivyobarikiwa
Ndani ya moyo wako binti nagonga murwa
Moto na moto yangu nikupe mapenzi moto moto
Amka usiendelee kulala njoo utimize ndoto

Murani wa kweli hivi hapa ningetoka tama
Mapito river kempo maskani ya kudumu
Leo Makini Jo si ukawahi hili gurudumu
Partner mzuri kwa hii biashara sitokudhulumu

Kula hata kama ni mbichi nyama kisha penda roho
Sikufichi maana utu uzima dawa
Uzoefu mwalimu mzuri na uzuri ni kwamba sijapagwa
Ni pendo tu, ni pendo tu kama Carola Kinasha
Gari umeniwasha binti we ni wa moto haswa
Ghetto men hapa kuwa gentlemen inapaswa

(Classic sound)

Walishazushaga kuniita kiwe-kiwembe
Sasa wametuliza mawe-mawenge
Umbea kwa vituo bama, vya mwenge
Habari zipo kwetu mnara wa wenge

Walishazushaga kuniita kicheche
Sasa wametuliza mawenge
Umbea kwa kituo bamaa vya mwenge
Yelele lile

Ninachomiliki hakinimiliki
Ila ninachomiliki haki ni miliki

Walishazushaga kuniita kiwe-kiwembe
Sasa wametuliza mawe-mawenge
Umbea kwa vituo bama, vya mwenge
Habari zipo kwetu mnara wa wenge

Made in Arusha, kabisa

Wananiita Mr Mstaarabu
Ninachongoja misa na ni sababu
Nishawekeza hisa ya hii dhahabu
Ndoa ndo imani msingi wa dhawabu

Walishazushaga kuniita kicheche
Sasa wametuliza mawenge
Umbea kwa kituo bamaa vya mwenge
Yelele lile

Walishazushaga kuniita kiwe-kiwembe
Sasa wametuliza mawe-mawenge
Umbea kwa vituo bama, vya mwenge
Habari zipo kwetu mnara wa wenge

Walishazushaga kuniita kicheche
Sasa wametuliza mawenge
Umbea kwa kituo bamaa vya mwenge
Yelele lile

Watch Video

About Kiwembe

Album : Kiwembe (Single)
Release Year : 2020
Copyright : (c) 2020
Added By : Huntyr Kelx
Published : May 03 , 2020

More JOH MAKINI Lyrics

JOH MAKINI
JOH MAKINI
JOH MAKINI
JOH MAKINI

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl