EMMANUEL MGOGO Napenda Niwe Karibu Na Wewe cover image

Napenda Niwe Karibu Na Wewe Lyrics

Napenda Niwe Karibu Na Wewe Lyrics by EMMANUEL MGOGO


Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga

Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga 

Maana hapa nilipo
Nipo moyoni na kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Napenda ooh, ninapendaga

Maana hapa nilipo
Sijaridhika nina kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Oooh ninapendaga

Nina haja na wewe bwana
Natamani ukae nami
Sioni mwingine bwana
Sijapata mwingine

Ila ni wewe wa kunifaa mimi
Wa kunitunza ila ni wewe
Tabibu wa karibu bwana
 
Usinipite pembeni bwana
Sina mwingine wa kunihurumia
Pale ninapo jeruhiwa
Na wanyang'anyi uwe karibu

We ni msamaria mwema utanihudumia
Utanifunga majeraha na kunifariji
Unionyeshe pendo lako
Maana wanipenda

Unionyeshe pendo lako
Maana wanipenda

Sioni la kunifurahisha
Nikiwa mbali na uwepo wako
Kama mti unang'olewa udongoni
Nitasinya na kudhoofika

Ninaomba univute niwe karibu nawe
Kama mti uliopandwa kando kando ya maji
Uzao wa matunda mazuri
Wala majani yake hayanyauki

Kila nitendalo nifanikiwe
Bwana naomba

Wewe ni maji ya uzima
Wewe ni maji yaliyo hai
Kisima cha uzima
Na upendo

Kama hayana na porini
Ayatamanivyo maji
Ndivyo nafsi yangu yakutamani wewe
Fanya hima usichelewe

Univute karibu nawe
Niwe na wewe

Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga

Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga 

Maana hapa nilipo
Nipo moyoni na kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Napenda ooh, ninapendaga

Maana hapa nilipo
Sijaridhika nina kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Oooh ninapendaga

Kukaa na wewe 
Ni shauku pekee 
Ya moyo wangu bwana aah
Hapa nilipo sijaridhika

Natamani nipandishwe juu
Univute karibu na wewe
Karibu zaidi ya jana
Uwe nuru uniangazie

Pendo lako kama maji
Nizame kwenye kisima 
Cha uwepo wako 

Nimesoma katika neno lako Zaburi
Umesema ooh
Aketiye mahali pake pa siri
Palipo juu 

Huyo atakaa katika uvuli wake mwenyezi
Ataokolewa na mitego ya adui
Silaha zote na mishale
Haitofanikiwa

Silaha zote na mishale
Haitofanikiwa

Nichue uniweke hapo bwana
Hili ni ombi la moyo wangu
Niketishe kwenye uwepo wako
Tuketishe kwenye uwepo wako

Usiniache gizani bwana
Peke yangu siwezi
Kaa nami, karibu nami
Ndani yangu nami ndani yako

Univute karibu nawe
Mikononi mwako niwe salama
Univute karibu nawe
Niwe na wewe bwana

Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga

Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga 

Maana hapa nilipo
Nipo moyoni na kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Napenda ooh, ninapendaga

Maana hapa nilipo
Sijaridhika nina kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Oooh ninapendaga

Watch Video

About Napenda Niwe Karibu Na Wewe

Album : Napenda Niwe Karibu Na Wewe (Single)
Release Year : 2019
Copyright : (c) 2019
Added By : Huntyr Kelx
Published : Nov 12 , 2019

More EMMANUEL MGOGO Lyrics

EMMANUEL MGOGO
EMMANUEL MGOGO

Comments ( 0 )

No Comment yet



About AfrikaLyrics

Afrika Lyrics is the most diverse collection of African song lyrics and translations. Afrika Lyrics provides music lyrics from over 30 African countries and lyrics translations from over 10 African Languages into English and French

Follow Afrika Lyrics

© 2024, We Tell Africa Group Sarl